Uchechemuzi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchechemuzi (kwa Kiingereza hujulikana kama Advocacy) ni kitendo au shughuli inayofanywa na mtu au kikundi cha watu kwa lengo la kushawishi mabadiliko katika sekta mbalimbali kama ngazi za maamuzi, siasa, uchumi, na masuala mengine ya kijamii.

Uchechemuzi unahusu pia shughuli mbalimbali zinazojumuisha masuala ya kisera, sheria na bajeti, zikiwa pamoja na taarifa za kweli, mahusiano pamoja na vyombo vya habari na kutuma ujumbe kwa serikali na jamii. Uchechemuzi unahusisha shughuli mbalimbali ambazo mtu au taasisi inazifanya, ikijumuisha pia kampeni katika vyombo vya habari, mazungumzo ya umma, machapisho ya kitafiti.

Katika uchechemuzi njia mbalimbali zinaweza kutumika, zikiwemo njia za kisheria.[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Lobbying Versus Advocacy: Legal Definitions. NP Action. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-04-02. Iliwekwa mnamo 2023-01-16.
Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uchechemuzi kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.