Sufi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kwa mwelekeo wa kidini tazama Sufii, Usufii
Sufi katika tunda la msufi mweupe, Ceiba pentandra, kisiwani Unguja
Msufi-pori (Rhodognaphalon schumannianum)

Sufi (kar. صوف suf[1]) ni jina kwa nyuzi laini kama pamba zinazotoka kwenye matunda ya msufi (miti ya jenasi Bombax, Ceiba na Rhodognaphalon).

Sufi hutumiwa kwa kujaza magodoro, kama kalafati kuziba nyufa kati ya mbao za mashua n.k. Haifai kwa kutengeneza nyuzi ndefu na vitambaa.

Mara nyingi neno hili linatumiwa pia kwa kutaja sufu yaani manyoya ya kondoo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. neno asilia katika Kiarabu صوف suf lamaanisha nywele manyoya laini ya kondoo na wanyama wengine limeingia katika Kiswahili kwa maumbo ya sufi na sufu