Stadi za lugha
![]() | Makala haina vyanzo vya kutosha
Makala (au sehemu ifuatayo ya makala) inatoa habari bila kuonyesha vyanzo au uthibitisho wowote.
|
Stadi za lugha ni zile mbinu ambazo mkufunzi anazitumia kufundisha lugha asilia kwa msomi wa lugha ya pili. Pia ni mbinu msomi wa lugha ya pili anazotumia kuhakikisha amempata mkufunzi wa lugha ya pili kiufasaha.
Stadi hizo pia zinaweza kuitwa mbinu za ufundishaji wa lugha ambazo nazo ni kama vile: kusikiliza na kuongea, kusoma, kuandika sarufi katika lugha funzwa na msamiati wa lugha funzwa.
Ni lazima mfundishaji wa lugha afuatilie utaratibu fulani ili aweze kuhakikisha wanafunzi wake wanampata ipasavyo. Mwalimu hawezi kufunza mwanafunzi kuandika kama hana ufahamu wa kusoma. Kwa hiyo, ni lazima afundishe mwanafunzi kusoma kwanza kabla ya kuchukua hatua ya kumfundisha jinsi ya kuandika.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Stadi za lugha kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |