Serikali ya Víchy

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Muonekano wa mji wa Vichy

Serikali ya Víchy ilitawala Ufaransa chini ya amri ya Ujerumani wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Iliongozwa na Jemadari Philippe Pétain na makao makuu yalikuwepo mjini Vichy katika kusini ya Ufaransa.

Petain alikubali kuunda serikali hii baada ya Ufaransa kushindwa na Ujerumani mwaka 1940. Kati ya Julai 1940 hadi Novemba 1942 serikali ya Vichy ilikuwa na mamlaka juu ya kusini ya Ufaransa ambako wanajeshi wa Ujerumani hawakuingia kufuatana na mapatano ya kusimamisha vita. Kaskazini ya Ufaransa ilikuwa chini ya amri ya kijeshi ya Kijerumani lakini hata hapa serikali ya Vichy ilikuwa na mamlaka ya kusimamia utawala wa miji na polisi ya Kifaransa.

Sehemu ya koloni za Ufaransa hasa katika Asia (Indochina) zilikubali mamlaka ya Vichy. Koloni katika Afrika zilifuata serikali ya "Ufaransa Huru" iliyoongozwa na Charles de Gaulle.

Tangu mwisho wa 1942 Ujerumani ulipeleka wanajeshi pia katika kusini ya nchi baada ya Wamarekani kufika Afrika ya Kaskazini na kutisha utawala wao katika kusini ya Ulaya.

Baada ya uvamizi wa maadui wa Ujerumani katika Ufaransa Kaskazini sehemu kubwa ya Wafaransa walisimama upande wa Charles de Gaulle na serikali ya Petain ilipaswa kukimbia Ujerumani. Maafisa wake walikamatwa huko 1945.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Serikali ya Víchy kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.