Nissan Skyline

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nissan Skyline (kwa Kijapani: 日産・スカイライン, Hepburn: Nissan Sukairain) ni aina ya gari iliyotengenezwa awali na kampuni ya Prince Motor kuanzia mwaka 1957 na baadaye na Nissan baada ya kampuni hizi kuungana. Baada ya kuunganishwa, Skyline na mwenza wake mkubwa zaidi, Nissan Gloria, ziliuzwa nchini Japani kwa njia za mauzo zinazoitwa Nissan Prince Shop.