Msaada:Futa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Futa ni amri ya kufuta ukurasa kwenye wikipedia. Inatekelezwa na wakabidhi ambao wanaweza pia kurudisha ukurasa uliofutwa kimakosa.

  • Kila mtumiaji anaweza kuondoa yaliyomo hata kuondoa kabisa na kuacha ukurasa tupu, isipokuwa hatakiwi kuondoa yote. Vilevile kila mtumiaji anaweza kurudisha maudhui yaliyofutwa.
  • Kuondoa maudhui ni tofauti na kufuta ukurasa wote, pamoja na historia yake na kurasa za majadiliano.
  • Kama ukurasa una maudhui ambayo hayafai kabisa (matangazo matupu ya kibiashara, lugha isiyo Kiswahili, Kiswahili kibaya mno, kukosa maana) unaweza kufutwa mara moja.
  • Kama ukurasa una kasoro nzito lakini inaweza kurekebishwa, inaweza kupewa alama ya {{futa}} kwenye mstari wa kwanza, halafu kuandikishwa kwenye ukurasa Wikipedia:Makala kwa ufutaji.
  • Kama ukurasa umefutwa kimakosa unaweza kurudishwa na mkabidhi yeyote kupitia Maalum:Usifute (restore).

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]