McDonald Mariga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pitio kulingana na tarehe 03:17, 11 Machi 2013 na Addbot (majadiliano | michango) (Bot: Migrating 21 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q313893 (translate me))
McDonald Mariga
Maelezo binafsi
Jina kamili McDonald Mariga Wanyama
Tarehe ya kuzaliwa 4 Aprili 1987 (1987-04-04) (umri 37)
Mahala pa kuzaliwa    Kenya
Urefu 1.88 m (6 ft 2 in)
Nafasi anayochezea Katikati
Maelezo ya klabu
Klabu ya sasa Internazionale Milano
Namba 17
Klabu za ukubwani
Miaka Klabu
2010 Internazionale Milano
Timu ya taifa
2006 Kenya

* Magoli alioshinda

McDonald Mariga Wanyama (amezaliwa tarehe 4 Aprili 1987) ni mchezaji wa mpira kutoka Kenya ambaye anaichezea kilabu cha Real Sociedad.

Wasifu katika Klabu

Mariga alianza kazi yake ya kucheza kandanda kwenye kilabu cha 'Ulinzi Stars' kabla ya kuhamia Pipeline FC. Mariga alikuwa mwanachama wa Shule ya Upili ya Kamukunji 'Golden Boys', ambayo mshambuliaji wa Kenya Dennis Oliech (Auxerre, Ufaransa) alikuwemo, na ilishinda mara mbili mfululizo kinyang'anyiro cha Mabingwa wa Taifa cha mwaka wa 2002 na 2003.

Mcheza kiungo cha kati huyu alienda Uswidi mwaka wa 2005 kuchezea upande wa tatu wa Division(Taarafa), Enköpings SK. Baada ya msimu mmoja tu katika ESK, yeye alitia saini kwa Helsingborgs IF kabla ya msimu wa 2006. Mafanikio yake katika Olympia yalikuwa ya haraka sana. Kufuatia madai ya awali ya meneja kutoka Portsmouth Harry Redknapp, Mariga alionekana akiwa tayari kuweka saini kwa timu hiyo ya Ligi Kuu, lakini masuala ya kibali cha kazi yalimzuia kwa kuwa yangegharimu karibu Yuro milioni mbili nukta saba.

Alihamia Serie A kilabu cha Parma FC kwa mkopo, mwezi wa Agosti mwaka wa 2007. Klabu hii ya Kiitaliano ilikuwa na chaguo la kumnunua katika majira ya joto kwa ada ya krona za Uswidi milioni 20 (karibu sawa na yuro milioni 2).[1] Mariga alikubali uamuzi wa miaka nne ya kuichezea Serie A upande wa Parma kwa miaka minne hadi mwisho wa Juni 2012, baada ya klabu kulipwa ada ya uhamisho ya Krona za Uswidi milioni 18 (takriban yuro milioni moja nukta tisa nne). Mpango huo, ulioandaliwa na aliyekuwa mchezaji nyota wa Uswidi, Martin Dahlin, sasa ni ajenti, unakosa Krona milioni 20 dhidi ya bei ya kuulizia ya awali iliyowekwa na Helsingborgs. Asilimia 25 ya ada ya uhamisho itaenda kwa Enkopings SK, klabu iliyotangulia kumleta Mariga Uswidi mwaka wa 2005.

Mariga, ambaye alikuwa na kipimo cha karibia Yuro milioni 0.8 kwa mwezi wa Julai mwaka jana alijiona bei yake ikiongeza hadi kwa takwimu iliyoko hivi sasa katika mwaka mmoja tu baada ya mafanikio yake katika Serie A ya Kiitaliano tangu ahamie huko kutoka Helsingborgs mwishoni mwa kufungwa kwa wakati wa Ulaya wa kusajili wachezaji mnamo Agosti iliyopita.

Mariga alichezea Parma mara 35 katika Serie B wakati wa msimu wa 2008-2009 huku akifunga mara tatu na kuwasaidia kurudi Serie A kwa msimu wa 2009-2010.

Wasifu wa Kimataifa

Mariga alifunga bao lake la kimataifa la kwanza dhidi ya Swaziland ikicheza na Kenya tarehe 25/03/2007.

Marejeo

Viungo vya nje