Mauaji ya Akai Gurley

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Akai Gurley, mwanamume mwenye umri wa miaka 28, aliuawa kwa kupigwa risasi 20,Novemba, 2014, huko Brooklyn, New York City, Marekani, na ofisa wa Idara ya Polisi ya Jiji la New York. Maafisa wawili wa polisi, wakishika doria kwenye ngazi za Mamlaka ya Makazi ya Jiji la New York (NYCHA) katika nyumba  za Louis H. huko mashariki mwa New York, Brooklyn, waliingia kwenye ngazi zenye giza nene, zisizo na mwanga. Afisa Peter Liang, 27, alichomolewa bunduki yake. Gurley na mpenzi wake waliingia kwenye ngazi ya ghorofa ya saba, hatua kumi na nne chini yao. Liang alifyatua silaha yake; risasi iliruka ukuta na kumpata Gurley kifuani. Baraza la mahakama lilimtia hatiani Liang kwa mauaji ya bila kukusudia, ambayo baadaye mahakama iliyapunguza kuwa mauaji ya kihalifu.

Mnamo10 Februari , 2015, Liang alishtakiwa na mahakama kuu (wanaume saba na wanawake watano) [1] kwa kuua bila kukusudia, kushambulia na mashtaka mengine ya jinai (jumla ya makosa matano) [2] baada ya wanachama kuonyeshwa picha za nyumba hiyo ambayo haikuwa na mwanga na glock ya 9mm iliyotumika katika upigaji risasi

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Former NYPD Cop Peter Liang's Guilty Verdict Leaves a Community Divided (en). NBC News. Iliwekwa mnamo 2022-04-16.
  2. J. Weston Phippen (2016-02-12). A Guilty Verdict in the Akai Gurly Case (en). The Atlantic. Iliwekwa mnamo 2022-04-16.