Malengo endelevu

Malengo Endelevu (kwa Kiingereza: Sustainable Development Goals, kifupi: SDGs) ni mkusanyo wa malengo 17 yalopangiliwa kwa faida ya watu wote.[1]
Malengo endelevu yalianzishwa mwaka 2015 na Baraza kuu la Umoja wa Mataifa likiwa na malengo ya kufikiwa mwaka 2030, kama sehemu za ajenda za mwaka 2030.[2][3][4]
Malengo endelevu ni:
- Kutokomeza Umaskini
- Kukomesha Njaa
- Afya Njema na Ustawi
- Elimu Bora
- Usawa wa Kijinsia
- Maji Salama na Usafi
- Nishati Mbadala na Gharama Nafuu
- Kazi Zenye Staha na Ukuaji
- Viwanda Ubunifu na Miundo Mbinu
- Kupunguza Tofauti
- Miji na Jamii Endelevu
- Matumizi Uzalishaji Wenye Uwajibikaji
- Kuchukua Hatua Dhidi ya Mabadiliko ya Tabia Nchi
- Kuendeleza Uhai katika Maji
- Kulinda Uhai katika Ardhi
- Amani Haki na Taasisi Madhubuti
- Ushirikiano katika Kufanikisha Malengo
Marejeo
- ↑ dpicampaigns. About the Sustainable Development Goals (en-US).
- ↑ United Nations Official Document.
- ↑ Transforming our world: the 2030 Agenda for Sustainable Development. Iliwekwa mnamo 23 August 2015.
- ↑ Global Goals | Policy and advocacy (en-GB) (2017-09-25).