Majadiliano ya mtumiaji:Stefano Kaisavira

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Karibu bwana Stefano Kaisavira katika Wikipedia ya Kiswahili!! Hapa ni sehemu ya kuundia kamusi elezo huru iliyo kamili. Ukiwa una swali basi uliza tu, utajibiwa. Pia unaweza kupata msaada wa kuanzisha makala kwa kubonyeza hapa. Karibu sana...--"Mwanaharakati" (talk) 18:24, 1 Machi 2008 (UTC)[jibu]


Bwana Stefano nilifuta maandishi yako kwenye ukurasa Msaada:Yaliyomo kwa sababu haikulingana na jina la makala. Nimeihamisha badala yake kwenye ukurasa wako wa mtumiaji. Japa uku huru kuandika habari zako. Menginevyo unatakiwa kufuata mahsarti ya Kamusi Elezo. Karibu. --User_talk:Kipala 22:40, 1 Machi 2008 (UTC)[jibu]

Hata hivyo bado ata hitaji msaada zaidi kwakuwa hajui lolote kuhusu Wikipedia. Huyu bwana, anajua Kiswahili cha msingi, na nilimuomba ajiunge nasi ili aweze kuendeleza kamusi elezo hii ya Kiswahili. Kwa bahati nzuri, anajua Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa. Naona kwa-kujua lugha hizo itakuwa rahisi kwa yeye kusoma makala katika fr:wiki au en:wiki na kuzitafsiri kwa Kiswahili!! Ingawaje mwenyewe anasema Kiswahili chake si kizuri sana lakini sie tutamsaidia kusahihisha makosa madogomadogo. Vilevile akiwa hapa, atapata kukuza Kiswahili chake zaidi kwakuwa hapa hatuzungumzi Kiingereza wala Kifaransa-Kijerumani, yeye atakuwa mtu wa kuandika Kiswahili tu. Hivyo itamsaidia katika kukuza lugha hii... Natumai niko sahihi....--"Mwanaharakati" (talk) 06:41, 3 Machi 2008 (UTC)[jibu]

Asante kwa salamu[hariri chanzo]

Asante kwa salamu zako Bwana Stefano. Natumaini hujambo na uko salama huko Brussels. Twamfurahia kila Mswahili na mimi nafurahia hasa kumjua mtu wa Kongo! Karibu! --User_talk:Kipala (majadiliano) 16:24, 14 Machi 2008 (UTC)[jibu]