Kigezo:Picha ya wiki
Mandhari
Julius Nyerere (Butiama, 13 Aprili 1922 - London, 14 Oktoba 1999) alikuwa Rais wa kwanza wa Tanzania na Baba wa Taifa. Aliongoza Tanganyika tangu uhuru mwaka 1961 kama Waziri Mkuu, kisha baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964, aliongoza Tanzania kama Rais hadi 1985. Aliunda sera ya Ujamaa na Kujitegemea ambayo iliweka msisitizo kwenye usawa wa kijamii, elimu kwa wote na umoja wa kitaifa. Baada ya kustaafu urais, aliendelea kuishi kwa kuendeleza shughuli za kijamii na kilimo, na alifariki dunia kutokana na saratani ya damu tarehe 14 Oktoba 1999 akiwa London, na kuzikwa Butiama. Je ungependa kusoma zaidi kuhusu Mtu huyu? au ungependa kuchangia zaidi kuhusu mtu huyu? fungua Hapa
