Kidyangadi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kidyangadi (au Kidhanggati) ni lugha ya Kipama-Nyungan nchini Australia inayozungumzwa na Wadyangadi katika jimbo la New South Wales. Katika sensa ya mwaka 2006, kulikuwa na wasemaji wa Kidyangadi watano tu, lakini hao ni matokeo ya mradi wa kufufua lugha ya Kidyangadi. Maana yake, lugha iliachwa kuzungumzwa wakati wa miaka ya 1960; halafu mwaka 2000 shule ikaanzishwa kwa ajili ya kufundisha lugha ya Kidyangadi tena. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kidyangadi kiko katika kundi la Kiyidiny.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kidyangadi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.