John Githongo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
John Githongo Mnamo mwaka 2015

John Githongo (alizaliwa mwaka wa 1965) ni mwandishi wa zamani wa Kenya ambaye alichunguza vitendo vilivyohusiana na rushwa na udanganyifu katika nchi yake ya nyumbani , chini ya rais Mwai Kibaki,na baadaye alichukua nafasi rasmi za kiserikali kupambana na rushwa. Mwaka wa 2005 aliacha nafasi hiyo, na baadaye kuwakashifu mawaziri kwa udanganyifu wao.

Baba yake aliyeitwa Joe Githongo alikuwa na kampuni ya uhasibu, ambapo Rais Jomo Kenyatta alikuwa mmoja wa wateja wake [1] John Githongo lienda shule ya kifahari ya St Mary's School mjini Nairobi. Alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi na kufuzu katika miaka ya tisini [1] Pia alisomea uchumi na Falsafa katika Chuo Kikuu cha Wales kabla ya kurudi nyumbani Kenya. Kwa muda mfupi alifanya kazi kazi kama msimamizi mshauri na mtafiti kabla ya kuhamia katika uandishi [2] Katika jukumu hili aliandika sana gazeti la EastAfrican lililokuwa mjini Nairobi akishambuli ufisadi nchini Kenya chini ya utawala wa Moi.

SAREAT[hariri | hariri chanzo]

Katika mwaka wa 1998, Kikundi kisicho cha kiserikali cha mwanasayansi wa kisiasa Mutahi Ngunyi kilichojulikana kama - 'Series for Alternative Research in East Africa' (SAREAT) Kilishirikisha John Githongo kuhariri jarida la kikana kuhusu siasa na uchumi , madadala ya ya gazeti la Afrika mashariki. Jarida hilo lilimalizika baada ya ukaguzi ulioashiriwa na shirikisho lililoongoza kwa msaada litwaloFord Foundation na kupatikana kuwa kuna mambo yaliyokuwa si halali upande wa Ngunyi, ambaye alikuwa mkurugenzi mkuu wa SAREAT na Dk Jonathan Moyo, ambaye alikuwa afisa wa programu katika Ford Foundation shughuli za kukipatia raslimali kikundi hiki kisicho cha serikali. Wao wana wawili wamekuwa sued na suala bado ni mahakamani. Inajulikana kuwa shirikisho la Ford limekubali wito wa Githongo kuwa shahidi wa mashtaka katika kesi.

Katika mwaka wa 1999, Githongo alianzisha na kuendeleza sura ya Kenya katika uwazi wa kimataifa, Shirika lisilo la kiserikali la kupambana na rushwa na ammekuwa akifanya kazi katika shirika hili kwa muda [2]

Kwazo la Anglo Leasing[hariri | hariri chanzo]

Januari mwaka wa 2003 aliteuliwa na nafasi ya Katibu Mkuu wa Utawala Bora na Maadili na rais Kibaki, kwa harakati zake za kupambana na ufisadi. Alijiuzulu katika nafasi yake tarehe 7 Februari 2005 [3] bila sababu , ingawa iliripotiwa kuwa liona kuwa serkali haikujitolea kukomezufisadi na pia alikuwa alipokea vitisho vya kifo [4] Kama matokeo ya kujiuzulu kwake, misaada ya kimataifa kwa Kenya ilisimamishwa. Bado anabakia kusisitiza kwa nguvu dhidi ya ufisadi.

Tarehe 22 Januari mwaka wa 2006, Githongo alimtaja Makamu wa Rais Moody Awori kama mmoja wa wanasiasa wa wanne (wakiwa na Kiraitu Murungi, aliyekuwa waziri wa haki na sasa waziri wa nishati; Mwiraria Daudi waziri wa fedha na waziri wa zamani wa usafiri Chris Murungaru) kama waliohusika katika kashfa iliyokuwa na thamani ya dola milioni 600 - inajulikana kama kashfa ya Anglo Leasing. Pia alidai kuwa Rais Kibaki alikuwa makosa katika jambo hilo. Kashfa hii ilihusu tuzo la mkataba uliopewa kampuni ya Anglo-leasing - ambayo ni kampuni haikuwepo. Githongo alidai kuwa fedha zingeweza kusaidia serikali katia kampeni. Madai haya yalikanushwa na Awori na Murungaru na uchunguzi ukaahidiwa[5]

Uhamishoni[hariri | hariri chanzo]

Githongo alihamia Uingereza baada ya kudai kwamba kumekuwa na vitisho dhidi ya maisha yake [6] lakini anafikiria kurejea Kenya kutoa ushahidi katika kamati ya ufisadi[7] Alichukua cheo katika chuo cha Oxford (Memba Washirikisha Mkuu wa chuo cha St Antony's). Imebainika hivi karibuni kwamba yeye alichukua cheo kingine kama Visiting Fellow wa kituo cha utafiti wa maendeleo ya kimataifa iliyoko huko Ottawa. Katika mahojiano na Fergal Keane wa kipindi cha BBC cha Newsnight tarehe 8 Februari 2006, Githongo alieleza kuwa ana ushahidi iliyoandikwa mkandani ambayo inathibitisha kuwa Kiraitu Murungi alijaribu kuzuia uchunguzi wake [8][9] Murungi alipendekeza kuwa mkopo wa shilingi milioni 30 kwa baba yake kupitia wakili aliyeitwa A. H. Malik ulikuwa umenunuliwa na Anura Pereira, na angeweza kusamehewa kwa 'kwenda polepole' uchunguzi wa Anglo leasing. Anabainisha kwamba mwishoni mwa uchunguzi wake, yeye alifikia hitimisho ya kwamba kashfa ya Anglo leasing ilihusisha hata viongozi wakubwa, na hivyo kuhatarisha maisha yake. Anglo leasing, na kashfa nyingine zilizofanana, zilisemekana na baadhi ya watu kuwa yalikuwa fedha za kimagendo za kulipia ugombeaji wa NARC katika uchaguzi wa 2007. Huko Uingereza, Githongo kwa siku mbili alitoa ushahidi katika tume ya wabunge wa Kenya ambao walikuwa wakichunguza kashfa hio. Pande zote mbili zilikuwa chanya kuhusu matokeo ya mikutano.[10]

Angalia pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 The EastAfrican, 14 Februari 2009: 'Traitor' who stayed true to Kenya
  2. 2.0 2.1 Profile of John Githongo at World Economic Forum
  3. BBC News: Kenya's anti-graft czar resigns
  4. BBC News: Kenya graft fighter 'threatened'
  5. BBC News: Graft claims rock Kenyan cabinet
  6. BBC News: Kenya 'safe' for anti-graft czar
  7. BBC News: Kenya campaigner 'could return'
  8. BBC News: 'Taped evidence' in Kenya scandal (includes 3.3Meg PDF of Githongo's dossier - a blockbuster)
  9. BBC News: Githongo reassured after meeting
  10. BBC News: Githongo kuhakikishiwa baada ya mkutano

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]