Jasoni wa Kurene

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Jasoni wa Kurene (kwa Kigiriki Ἰάσων κυρήναιος) alikuwa Myahudi wa Kurene, Libya, aliyeishi katika karne ya 2 KK na kuandika historia ya vita vya ukombozi vya Wamakabayo hadi ushindi wao dhidi ya jemadari Nikanori (175 KK-161 KK).

Maandishi hayo yaliyopotea yalikuwa katika vitabu vitano lakini yalifupishwa na kurekebishwa na Myahudi mwingine asiyejulikana katika kitabu kilichopo hadi leo maarufu kama Kitabu cha pili cha Wamakabayo, kimojawapo cha vitabu vya Deuterokanoni katika Biblia ya Kikristo ya madhehebu kadhaa. Tazama 2 Mak 2ː24.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jasoni wa Kurene kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.