Ike Diogu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ikechukwu Somtochukwu Diogu (alizaliwa Septemba 11, 1983) ni mchezaji wa Marekani mwenye asili ya Nigeria na mtaalamu wa mchezo wa kikapu basketball akichezea timu ya Shimane Susanoo Magic ya ligi B.

Familia na maisha ya Awali[hariri | hariri chanzo]

Wazazi wa Diogu ni Wanigeria, waliohamia nchini Marekani mwaka 1980 kwa ajili ya masuala ya kielimu. Baadae walihamia katika mji wa Buffalo, New York, na kisha mji aliozaliwa wa Garland, Texas. Ike alihudhuria Austin Academy, na kisha kuandikishwa katika shule ya upili ya Garland High School.

Diogu ni mwanachama wa kabila la Waigbo.[1]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Kirkpatrick, Curry. Plenty to like about Ike. ESPN Internet Ventures. Iliwekwa mnamo 2009-01-25.
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ike Diogu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.