Godfrey Calvin Magila

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Godfrey Calvin Magila (alizaliwa mkoani Mbeya, 28 Februari 1992 [1]) ni mhasibu kwa Taaluma na ni Mwana TEHAMA mwanzilishi wa Kampuni ya Magilatech ambayo inajihusisha na kutengeneza mifumo mbali mbali ya Kompytuta . Magila ni mmoja kati ya vijana walio anzisha makampuni wakiwa na umri mdogo ndani ya Tanzania na kuweza kufanikiwa.

Maisha Yake[hariri | hariri chanzo]

Akiwa na umri wa miaka 5 Godfrey alipata pigo la kufiwa na mama yaje mzazi ingawa hakuwahi kulelewa na baba mzazi kwani alifariki Godfrey akiwa na umri wa miezi mitatu tu kutoka azaliwe. Akalelewa na ndugu zake kuanzia mwaka 1998 ambapo mwaka 2010 na mwaka 2011 ukawa ni mwaka mwingine wenye pigo kwake kwa kupoteza walezi wake wote wawili walio mlea[2].

Elimu Yake[hariri | hariri chanzo]

Alisoma shule ya Mbezi Beach High School iliyopo jijini Dar es salaam. Mwaka 2010 alijiunga na chuo kikuu cha IFM kusomea kozi ya uhasibu.

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Magilatech Tanzania, Congo, Dubai. Kupitia kampuni yake ya Magilatech, Godfrey amekuwa akitengeneza mifumo katika makampuni na Taasisi ndani na nje ya Tanzania ambapo pia amefungua Kampuni ndani ya Dubai[3] na kuajiri wafanyakazi wengi kutoka nchi mbali mbali. Serikali ya Tanzania inamtambua kama ni kijana mwenye mchango mkubwa na inajivunia. “Kuna vijana wametoka wazuri katika hii mifumo yetu chukua mfano kuna kijana anaitwa Magila kutoka Magilatech yeye ameanza na Costech (Atamizi ya Tume ya Science na Technolojia) yuko DRC anatengeneza mifumo ni kijana wa kitanzania” - Rais Samia Suluhu Hassan[4]

Tuzo na Teuzi[hariri | hariri chanzo]

  1. Start-up World Africa - Top Ten Finalist (2012)
  2. Innovation Fund  award  for best app (2014)
  3. Global Recognition  Of Excellence - ITU Hungary (2015)
  4. 30 Under 30 By Forbes (2017)
  5. Innovator of the year - All Africa Bussiness Learders ( Awards AABLA ) - East Africa (2017)
  6. Top100 midsized Companies By KPMG, The Citizen (2018)

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.startupgrind.com/events/details/startup-grind-dar-es-salaam-presents-godfrey-magila-magilatech-company-ltd/
  2. https://www.thecitizen.co.tz/tanzania/magazines/success/how-a-passionate-gamer-built-a-tech-company-3799654
  3. https://millardayo.com/magiladubai/
  4. https://millardayo.com/rais-samia-atambua-mchango-mkubwa-wa-magila-tech-aeleza-mipango-ya-serikali-katika-hili/

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

  1. https://wsa-global.org/person/3535/
  2. https://talkafricana.com/forbes-africa-list-of-30-under-30-most-promising-young-african-entrepreneurs-2017/
  3. https://www.thecitizen.co.tz/tanzania/magazines/success/tanzania-s-top-tech-players-share-pathways-to-success-4098672
  4. https://www.bellanaija.com/2017/06/forbes-africa-30-under-30-2017-list-see-young-entrepreneurs-doing-great-things/