Bashir Abdi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Abdi kwenye Mashindano ya Riadha ya Uropa ya 2018
Abdi kwenye Mashindano ya Riadha ya Uropa ya 2018

Bashir Abdi (amezaliwa 10 Februari 1989) ni mwanariadha wa Ubelgiji mzaliwa wa Somalia ambaye ni mtaalamu wa mbio za masafa marefu.

Alishinda medali ya shaba katika mbio ya Marathoni kwenye Olimpiki ya mwaka 2020. Pia alikuwa mshindi wa medali ya fedha katika Mashindano ya Riadha ya Ulaya mwaka 2018 katika shindano la mita 10,000[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Bashir ABDI | Profile | World Athletics". worldathletics.org. Iliwekwa mnamo 2021-11-28.