Admirali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kola, bega, na nembo ya alama kwa Admiral katika Jeshi la Wanamaji la Merika

Admerali (pia: admeri, admirali) ni cheo cha kiongozi mkuu wa kijeshi wa wanamaji. Cheo hicho kinalingana na jenerali katika matawi mengine ya jeshi.

Neno linatokana na Kiarabu أمير البحر amir-al-bahr yaani "mwenye mamlaka baharini". Iliingia katika lugha za Ulaya kama "admiral".

Cheo hicho si kawaida katika jeshi la majini la Tanzania wala Kenya, lakini hutumiwa kutafsiri vyeo vya kigeni[1].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Linganisha "Admeri", katika Kamusi Kuu ya Kiswahili, Longhorn - Bakita 2016, ISBN 9789987020984