Yaunde

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Jiji la Yaounde
Nchi Kamerun
Mahali pa Yaoundé katika Kamerun
Yaoundé

Yaoundé ni mji mkuu na mji mkubwa wa pili nchini Kamerun baada ya Douala. Ina wakazi 1,299,369 (2021[1]

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Mji uko kwenye kimo cha 730 m juu ya UB katika vilima vya Kamerun ya magharibi takriban 160 km kutoka mwambao wa Atlantiki. Hali ya hewa ni ya kitropiki; halijoto ina wastani ya 23.3 C°. Mvua hunyesha Septemba / Oktoba na Aprili / Mei.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Yaounde ilianzishwa mwaka 1888 BK na wanfanya biashara Wajerumani. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia na mgawanyo wa nchi ikawa sehemu ya Kamerun ya Kifaransa na mji mkuu wa koloni kuanzia mwaka 1922. Wakati wa uhuru mwaka 1961 ilikuwa mji kuu wa Kamerun yote pamoja na sehemu zilizokuwa chini ya Uingereza.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Yaounde ni kitovu cha usafiri na mawasiliano ya nchi. Kuna viwanda vya tumbako, vyakula, vioo na ubao. Yaounde ni kitovu cha biashara kwa ajili ya kilimo cha kahawa, kakao, nguta na raba katika mazingira ya mji. Kuna pia migodi ya dhahabu na metali ya titani.

Waliozaliwa Yaounde[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Yaunde kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.