Wilaya ya Kinondoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Kinondoni (kijani cheusi) katika mkoa wa Dar es Salaam.
Picha ya angani ya Wilaya ya Kinondoni mnamo mwaka 2015.

Wilaya ya Kinondoni ni mojawapo ya wilaya 5 za Mkoa wa Dar es Salaam yenye postikodi namba 14000. Kwa lugha nyingine ni manispaa ndani ya jiji la Dar Es Salaam.

Eneo lake ni sehemu za kaskazini za jiji. Kinondoni inaanza upande wa pwani kwenye Selander Bridge juu ya mto Upanga (pia: Msimbazi Creek) na kuendelea kupitia rasi ya Msasani, Kunduchi hadi Mbweni pamoja na hoteli za kitalii zilizopo sehemu hizo.

Barani inaelekea kuvukia barabara ya Morogoro hadi Mbezi na Kibamba. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kipo ndani ya manispaa hii.

Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa Kinondoni ilihesabiwa kuwa 1,775,049 [1]. Baada ya wilaya kumegwa, katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa 982,328 [2].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Sensa ya Tanzania ya 2012. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-02-10. Iliwekwa mnamo 2010-10-30.
  2. https://www.nbs.go.tz

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Kinondoni - Tanzania

BunjuHananasifKaweKigogoKijitonyamaKinondoniKunduchiMabwepandeMagomeniMakongoMakumbushoMbezi JuuMbweniMikocheniMsasaniMwananyamalaMzimuniNdugumbiTandaleWazo