Rasi ya Iberia
Kutoka Wikipedia
Rasi ya Iberia ni kati ya rasi kubwa za Ulaya ikiwa na eneo la 582,860 km². Iko katika kusini magharibi ya Ulaya ikipakana na Bahari Atlantiki upande wa kazkazini na magharibii halafu Bahari Mediteranea upande wa kusini na mashariki. Milima ya Pirenei ni mpaka kati ya rasi na Ulaya ya magharibi yaani Ufaransa.
Iberia ni jina la kale tangu zamani za Waroma wa Kale.
[hariri] Nchi na maeneo
Kwenye rasi kuna nchi zifuatazo:
- Hispania ni nchi kubwa kwenye rasi
- Ureno iko upande wa magharibi
- Andorra ni nchi ndogo sana katika milima ya Pirenei kati ya Hispania na Ufaransa
- Gibraltar ni eno ndogo la Uingereza katika kusini inayotazama Afrika.

