Nyang'aranga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Nyang'aranga ni kijiji kilichopo ndani ya kata ya Mugeta, tarafa ya Chamriho iliyoko wilaya ya Bunda, mkoa wa Mara.[1].

Jamii ya kijiji hiki wengi wao ni wa kabila la Wakurya na hujishughulisha na kilimo pamoja na ufugaji.

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 walianza kuchanganyika kwa wiki na watu kutoka sehemu mbalimbali, na hii ni baada ya kupiga hatua kiuchumi japo bado asilimia kubwa ni maskini kwani hutegemea mvua katika kilimo, ufugaji na hata maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Kumbe kijiji hiki ni miongoni mwa vijiji vingi nchini Tanzania vinavyokumbwa na ukame.

Nyang'aranga ina shule ya msingi.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]