Kimeng'enya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Modeli ya kimeng'enya kinachoitwa TIM.

Vimeng'enya (kwa Kiing. enzyme) ni molekuli za pekee za kibiolojia zinazojengwa na mwili ambazo kazi yake ni kuharakisha michakato ya kikemia mwilini. Mara nyingi ni protini. Inafanya kazi kama kichochezi kinachoharakisha mmenyuko wa kikemia. Kwa hiyo vimeng'enya vinasaidia kazi za mwilini kama mmeng'enyo wa chakula.

Mfano wake ni kimeng'enya cha amylasi kinachopatikana katika mate mdomoni. Kimeng'enya hicho kinavunja molekuli za wanga kuwa molekuli ndogo zaidi. Hizo molekuli ndogo zaidi zinaendedela kuvukwa tumboni lakini kazi ya tumbo imesharahisishwa kutokana na kimeng'enya katika mate.

Kuna pia vimeng'emya nje ya mmeng'enyo tumboni: vina kazi kote mwilini ndani ya seli, kwa mfano vinaendesha kunakiliwa kwa DNA wakati wa kuzaa.

Vimeng'enya vimepata kazi pia katika bioteknolojia. Hapo vinatengenezwa katika maabara au hata viwandani ama kwa kutumia bakteria wa pekee au kwa kuiga mchakato wa bakteria kwa mbinu za kikemia.

Kwa mfano vimeng'enya vinatiwa katika sabuni ya kufulia nguo ili kuharakisha kuondolewa kwa mafuta au damu.

Viungo vya Nje

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kimeng'enya kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.