Erie (ziwa)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ziwa Erie
Ziwa Erie (buluu nyeusi) kati ya maziwa makubwa

Ziwa Erie ni moja ya maziwa makubwa ya Amerika ya Kaskazini. Pamoja na maziwa mengine ya Ziwa Superior, Ziwa Huron na Ziwa Ontario liko mpakani kati ya Marekani na Kanada na mpaka huu umepita ziwani.

Ziwa limepakana na Kanada (jimbo la Ontario) upande wa kaskazini halafu na Marekani (majimbo ya Ohio, Pennsylvania, New York na Michigan) upande wa kusini na magharibi. Jina limetokana na kabila la Waerie walioishi hapa kabla ya kuingia kwa Wazungu.

Ziwa Erie hupokea maji yake kutoka Ziwa Huron kupitia mto Detroit. Kuna pia mito mingine inayoishia moja kwa moja ziwani. Maji hutoka kwa nia ya mto Niagara kwenda Ziwa Ontario. Maporomoko ya Niagara yako kati ya maziwa Erie na Ontario.

Vipimo[hariri | hariri chanzo]

Ziwa lina urefu wa kilomita 388 na upana mkubwa wa 92 km. Uso wake una eneo la 25,744 km². Kina cha wastani ni 19 m lakini kina kikubwa chafikia 64 m.

Maziwa Makubwa[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Kanada bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Erie (ziwa) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Makala hii kuhusu maeneo ya Marekani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Erie (ziwa) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.