Dominica Dipio

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Dominica Dipio (kitaaluma anajulikana kama Profesa Sista Dominic Dipio) ni mtawa Mkatoliki wa Uganda, mtengenezaji wa filamu, mwandishi na profesa wa Fasihi na Filamu katika Chuo Kikuu cha Makerere huko Kampala, Uganda[1][2][3]. Kama dada, yeye ni wa Taasisi ya Masista Wamishonari wa mama wa kanisa la MSMMC, mkutano wa kidini ulioanzishwa na Uganda katika jimbo Katoliki la Lira kaskazini mwa Uganda[4]. Mnamo Novemba 2019 aliteuliwa mshauri wa Baraza la Kipapa la Utamaduni na Papa Francis.[5][6]

Historia na Elimu[hariri | hariri chanzo]

Dipio alizaliwa Adjumani katika mkoa wa Magharibi mwa Nile nchini Uganda. Alihudhuria shule ya wasichana wa Saint Mary, Aboke, kwa elimu yake ya sekondari kabla ya kuendelea na chuo cha Trinity Nabbingo kwa elimu yake ya juu. Baadaye alihudhuria chuo kikuu cha Makerere na kupata shahada ya Sanaa katika elimu na kisha shahada ya uzamili ya fasihi. Mnamo 1991, Dipio alichukua cheti katika masomo ya wanawake katika kitivo cha sayansi ya jamii wakati huo katika chuo kikuu cha Makerere. Mnamo mwaka 2004, alimaliza shahada yake ya uzamizi katika masomo ya filamu katika chuo kikuu cha kipapa cha Gregorian huko Roma.Wakati huo huo alihutubia juu ya utangulizi wa ukosoaji wa filamu na sinema ya kiafrika katika chuo kikuu hicho hicho alipokuwa akisoma masomo yake.Mnamo mwaka wa 2010, aliteuliwa kuwa makamu wa rais wa jumuiya ya mafunzo ya kiafrika ya Rutgers.

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Katika taaluma, Dipio ni profesa wa fasihi na mnamo 2007 aliteuliwa kuwa mkuu wa idara ya Fasihi katika chuo kikuu cha Makerere, na kumfanya kuwa mwanamke mkuu wa kwanza wa kiafrika wa idara hiyo.Pia aliwahi kuwa mshauri wa ukuzaji wa mtaala haswa wakati chuo kikuu cha Uganda cha Kyambogo, kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), kilikuwa kikijiandaa kuandaa mtaala wa urithi wa kitamaduni.

Dipio anahusika katika tasnia ya filamu ya Uganda akiwa ameongoza na kutengeneza filamu na maandishi kadhaa. Amewahi kuwa jaji na mwanachama wa majaji katika sherehe kadhaa za filamu kama vile Tamasha la Filamu la kimataifa la Zanzibar (ZIFF) mnamo 2011, Tamasha la Filamu la Amakula, na aliwahi kuwa jaji mkuu katika uzinduzi wa Tamasha la Filamu la Uganda mnamo 2013 na vile vile kwa wengine baada ya hapo.

Mnamo Februari 2019, Dipio alikuwa mmoja wa wahudumu katika Tuzo za Filamu za Kiekumeni kwenye tamasha la filamu la Berlinale huko Ujerumani. Tuzo ya kila mwaka ya filamu ya Kiekumene ambayo ilikuwa katika mwaka wake wa 27 iliandaliwa na Shirika la Kimataifa la Filamu la Interchurch (Interfilm) na Jumuiya ya Mawasiliano ya Kikatoliki Ulimwenguni (SIGNIS).

Kabla ya kuteuliwa kama Mshauri, Dipio aliwahi kuwa mmoja wa washauri kadhaa kwa baraza la kipapa la mawasiliano ya jamii huko Vatican wakati wa uteuzi wa Papa Benedict XIV mnamo 2011.Wakati huo huo alikuwa mwanachama wa kamisheni ya mawasiliano ya jamii ya baraza la maaskofu la Uganda.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Prof. Dominica Dipio". llc.mak.ac.ug (kwa Kiingereza). School of Languages, Literature and Communication, CHUSS. Iliwekwa mnamo 2 July 2020.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Maractho, Emilly Comfort. "No higher honour for Prof Dominic Dipio", 25 November 2019. Retrieved on 2020-10-17. Archived from the original on 2020-06-29. 
  3. "Dominica Dipio". Who's Who in Research: Media Studies (kwa Kiingereza). Intellect Books. 2013. ISBN 978-1-78320-160-0. Iliwekwa mnamo 7 July 2020.  Check date values in: |accessdate= (help)
  4. "Home page" (kwa en-gb). Missionary Sisters of Mary Mother of the Church. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-10-18. Iliwekwa mnamo 2 July 2020.  Check date values in: |accessdate= (help)
  5. "Resignations and Appointments". press.vatican.va. Iliwekwa mnamo 2020-07-01. 
  6. "Ugandan Nun Appointed Consultor of Pontifical Council for Culture Feels "humbled, honored"". News (kwa en-gb). Missionary Sisters of Mary Mother of the Church. 10 November 2019. Iliwekwa mnamo 2 July 2020.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dominica Dipio kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.