Demi Moore

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Demi Moore

Demi Moore mnamo 2010
Amezaliwa Demi Gene Guynes
11 Novemba 1962 (1962-11-11) (umri 61)
Roswell, New Mexico, US
Kazi yake Mwigizaji
Miaka ya kazi 1982–hadi sasa
Ndoa Freddy Moore (1982–1985)
Bruce Willis (1987–2000)
Ashton Kutcher (2005–2013)

Demi Gene Guynes (amezaliwa tar. 11 Novemba 1962) anafahamika kwa jina la kikazi kama Demi Moore, ni mwigizaji wa filamu kutoka nchini Marekani.

Baada ya nyusika ndogondogo katika filamu na maigizo ya vipindi vya televisheni General Hospital, Moore amekuza kazi yake katika filamu kama vile St. Elmo's Fire (1985) na Ghost (1990) na mwanzoni mwa miaka ya 1990 amekuwa miongoni mwa waigizaji wa kike wenye kulipwa mapesa mengi sana katika Hollywood kwa kufuatia mafanikio yake katika filamu kama vile A Few Good Men (1992), Indecent Proposal (1993) Disclosure (1994). The Hunchback of Notre Dame (1996) na G.I. Jane (1997). Mwishoni mwa miaka ya 1990 filamu zake zilikuwa na mafanikio machache, lakini amerudi tena katika umaarufu na uhusika wake katika Charlie's Angels: Full Throttle (2003).

Moore amechukua jina lake la kikazi kutoka kwa mume wake wa kwanza Freddy Moore na ni mama wa watoto watatu kutoka katika ndoa yake na Bruce Willis. Baada ya kuolewa na mwigizaji Ashton Kutcher mwaka 2005 alibadili jina lake la mwisho kuwa Kutcher mnamo 2009.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani wa Marekani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Demi Moore kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.