Chekehukwa
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Chekehukwa | ||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
|
Chekehukwa ni ndege wa familia ya Burhinidae. Ndege hawa wana rangi zinazowanyerereza wakisimama au kutembea chini. Wakiona hatari husimama tuli na hupatana na mahali pa nyuma. Kwa hivyo hawaoneki sana wakati wa mchana. Huenda zaidi usiku na huoneka mara kwa mara mwangani kwa mbele kwa gari. Husikika zaidi ya kuoneka. Wanatokea maeneo makavu na hula wadudu, mijusi na wanyama wadogo.
[hariri] Spishi za Afrika (na Ulaya)
- Burhinus capensis, Chekehukwa Madoa (Spotted Thick-knee or Spotted Dikkop)
- Burhinus oedicnemus, Chekehukwa wa Ulaya (Stone-curlew)
- Burhinus senegalensis, Chekehukwa Magharibi (Senegal Thick-knee)
- Burhinus vermiculatus, Chekehukwa-maji au Chekeamwezi (Water Thick-knee or Water Dikkop)
[hariri] Spishi za mabara mengine
- Burhinus bistriatus (Double-striped Thick-knee)
- Burhinus grallarius (Bush Stone-curlew)
- Burhinus superciliaris (Peruvian Thick-knee)
- Esacus giganteus (Beach Stone-curlew)
- Esacus recurvirostris (Great Thick-knee)