Bata mkia-ngumu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Bata mkia-ngumu
Bata kichwa-cheupe
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Anseriformes (Ndege kama mabata)
Familia: Anatidae (Ndege walio na mnasaba na mabata)
Nusufamilia: Oxyurinae (Mabata mkia-ngumu)
Jenasi: Biziura Stephens, 1824

Heteronetta Salvadori, 1865
Nomonyx Ridgway, 1880
Oxyura Bonaparte, 1828

Mabata mkia-ngumu ni ndege wa maji wa nusufamilia Oxyurinae katika familia Anatidae. Manyoya ya mkia wao ni makavu na yametandawaa mara nyingi. Rangi ya dume ni kahawia au kahawiachekundu na domo lake lililovimba msingini ni buluu; jike ni mweusi au kijivu wenye domo la rangi ile ile. Spishi hizi huzamia kabisa ili kutafuta chakula. Hula mimea na invertebrata ya maji. Miguu yao iko nyuma sana, kama ile ya mabata wazamaji, ili kujisogeza mbele vizuri ndani ya maji. Kwa sababu hiyo hawawezi kutembea vizuri. Hujenga tago lao ndani ya uoto mzito wa maji. Jike huyataga mayai 3-8, lakini pengine hadi mayai 12 yanapatikana kwa sababu jike mwingine ameongezea mayai yake.

Yaliyomo

Spishi za Afrika [hariri]

Spishi za mabara mengine [hariri]

Spishi ya kabla ya historia [hariri]

  • Biziura delautouri (De Lautour's or New Zealand Musk Duck, Holocene ya New Zealand)
  • Tirarinetta kanunka (Piocene ya Australia Kusi)

Picha [hariri]