Uuaji wa Ramarley Graham

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uuaji wa Ramarley Graham ulifanyika katika mtaa wa Bronx, jiji la New York mnamo Februari 2, 2012.

Richard Haste, afisa wa Idara ya polisi ya New York, alimpiga risasi Graham katika bafu la nyumba ya marehemu. Graham mwenye umri wa miaka 18 alikuwa na bangi wakati afisa Haste alipojaribu kumzuia barabarani. Graham alikimbilia kwenye nyumba ya mama yake mkubwa, na akaingia bafuni kutupa bangi. Afisa Haste alijilazimisha kuingia ndani ya jengo hilo, akaupiga teke mlango wa mbele kisha akavunja bafu, ambapo alimpiga risasi Ramarley Graham hadi kufa. Haste aliweza kuonekana kwenye kamera za uchunguzi akitabasamu na kucheka pamoja na maofisa na wapelelezi—wanaume walewale ambao wangetoa ushahidi baadaye walikuwa wamemwambia Haste kwamba Graham alikuwa na bunduki. Haste alidai kuamini kwamba Graham amekuwa akitafuta bunduki kwenye kiuno chake, lakini hakuna silaha iliyopatikana.[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. MATTHEW LYSIAK, Daniel Beekman, Larry McShane. Cops cheer NYPD Officer Richard Haste, charged in death of teen Ramarley Graham. nydailynews.com. Iliwekwa mnamo 2022-04-16.