Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 2004

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 2004 ulikuwa wa 55 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 2 Novemba. Upande wa "Republican Party", Rais George W. Bush (pamoja na kaimu wake Dick Cheney) alimshinda mgombea wa "Democratic Party" John Kerry (pamoja na kaimu wake John Edwards).

Matokeo[hariri | hariri chanzo]

Bush akapata kura 286, na Kerry 251, wakati mchaguzi mmoja akampigia kura Edwards badala ya Kerry. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.