Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1988

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1988 ulikuwa wa 51 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 8 Novemba. Upande wa "Republican Party", mgombea George H. Bush (pamoja na kaimu wake Dan Quayle) alimshinda mgombea wa "Democratic Party" Michael Dukakis (pamoja na kaimu wake Lloyd Bentsen).

Matokeo[hariri | hariri chanzo]

Bush akapata kura 426, na Dukakis 111 wakati mchaguzi mmoja kutoka West Virginia alimpigia kura Bentsen badala ya Dukakis. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.