Tuzo zote za Muziki Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Tuzo za Muziki Afrika (AFRIMA) Ni tukio la kila mwaka la utoaji tuzo, tuzo hizi zilianzishwa na kamati ya kimataifa ya AFRIMA, wakishirikiana na umoja wa Afrika (AU) kwa ajili ya kutunza na kuwapongeza wasanii, vipaji na ubunifu katika bara la Afrika, kusambaza na kukuza urithi na utamaduni wa Afrika, onyesho lake la tuzo za waanzillishi lilifanyika mnamo 2014.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Nigeria imeandaa matoleo matatu ya tuzo wakati wa 2014-2016. Nigeria kwa mwaka mwingine ilishinda mwaka wa nne waumiliki wa haki za kuandaa tuzo mnamo mwaka 2017.[1][2]

Hata hivyo, Jamhuri ya Ghana ilipewa haki ya kuandaa Tuzo za (All Africa Music Awards) kwa miaka minne mfululizo kuanzia Desemba 2018 hadi 2020. Siku ya Jumatatu, Julai 15, 2019, Kamati ya Kimataifa ya Tuzo za Muziki wa Afrika (AFRIMA), iliondoa haki za uenyeji kutoka Jamhuri ya Ghana kwa matoleo ya 2019 na 2020 ya Tuzo za All Africa Music Awards, AFRIMA, kwa kukosa uwezo wa Nchi Mwenyeji kukidhi majukumu ya kifedha na kimkataba yaliyowekwa mnamo Julai 12, 2018, muhimu ili kudumisha uenyeji. tukio kubwa zaidi la muziki barani Afrika.[3] Kwa sababu ya mlipuko wa Covid-19 mnamo 2020, (AFRIMA) haikufanya kama ilivyopangwa lakini ilirejea mnamo 2021 na iliandaliwa Lagos, Nigeria.

  1. https://thenationonlineng.net/nigeria-to-host-music-award/
  2. https://dailypost.ng/2017/09/11/nigeria-host-afrima-2017-2019/
  3. https://pmexpressng.com/ghana-lost-afrima-hosting-rights/