Tanja Gönner

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Tanja Gönner ni mwanasiasa wa Ujerumani na mwanachama wa Muungano wa Kidemokrasia wa Kikristo wa Ujerumani( Christian Democratic Union of Germany).

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Tanja Gönner alizaliwa huko Sigmaringen, Baden-Württemberg, Ujerumani. [1] Gönner alisoma Liebfrauenschule, shule ya wasichana ya Kirumi-Katholiki. Alisomea ukarani wa sheria katika huduma ya mahakama kuu. [2] Alisomea sheria Chuo Kikuu cha Tübingen . Baada ya kumaliza mtihani wa kwanza na wa pili wa sheria wa serikali, alimaliza mafunzo yake ya kisheria katika Mahakama ya Mkoa ya Ravensburg . Kuanzia 1996 hadi 1999, alifanya kazi katika kampuni ya wanasheria huko Bad Saulgau . Baada ya kupata kibali cha kufanya kazi kama wakili, alikua mshirika katika kampuni hiyo ya mawakili mwaka wa 1999 na kufanya kazi huko kwa kuzingatia sheria ya ufilisi hadi 2004. [2]

Siasa[hariri | hariri chanzo]

Gönner alianza kazi yake ya kisiasa mwaka 1986 Junge Union, shirika la vijana la CDU. Amekuwa mwanachama wa CDU tangu 1987, na alikuwa mwanachama wa kamati kuu ya shirikisho kutoka 2000 hadi 2012. Kuanzia 2002 hadi 2004 Gönner alikuwa mwanachama wa Bundestag ya Ujerumani.

Mnamo mwaka 2004 alikua Waziri wa Masuala ya Kijamii wa Jimbo la Baden-Württemberg kwenye serikali ya Erwin Teufel . Mnamo 2005 alichukua Wizara ya Mazingira huko Baden-Württemberg kwenye baraza la mawaziri la Günther Oettinger, ambapo aliongoza hadi mapema 2010.

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tanja Gönner kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  1. Fricker, Uli (2019-12-26). "Baden-Württemberg: Die Weltverbesserin: Was macht eigentlich ... Tanja Gönner?". SÜDKURIER Online (kwa Kijerumani). Iliwekwa mnamo 2021-12-27. 
  2. 2.0 2.1 "Tanja Gönner - Munzinger Biographie". www.munzinger.de. Iliwekwa mnamo 2021-12-27.