Mzunguko wa moyo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Moyo matukio yanayotokea katika mzunguko wa moyo. Mizunguko miwili kamili ni michoro.

Mzunguko wa moyo (pia: mwendo wa moyo[1]; ing. cardiac cycle) inamaanisha matukio yote au yoyote kuhusiana na mtiririko au shinikizo la damu ambayo hutokea kuanzia mwanzo wa pigo la kwanza la moyo hadi mwanzo wa pigo la pili. [2] Idadi ya mizunguko ya moyo kwa sekunde ni kasi ya kupiga kwa moyo. Kila pigo la moyo lina hatua tano muhimu: la kwanza, "dayastoli ya baadaye", ni wakati vali za semilunar hufunga, na vali za atrioventricular (AV) hufunguka, na moyo mzima umepumzika. Ya pili, "sistoli ya atiria", ni wakati atiria hunywea, vali za AV hufunguka, na damu hutiririka kutoka atiria kwenda ventrikali. Ya tatu, "mnyweo wa ventrikali ulio na mjao sawa", ni wakati ventrikali hunywea, na vali za AV na zenye umbo la nusu mwezi (semilunar) hufunga, na hakuna mabadiliko katika kiasi cha damu. Ya nne, "Ufukuzo wa ventrikali", ni wakati ventrikali ni tupu na zinanywea, na vali za semilunar ziko wazi. Kwenye hatua ya tano, "Kupumzika kwa ventrikali kwa mjao sawa", shinikizo hupungua, hakuna damu inayoingia kwenye ventrikali, ventrikali huacha kunywea na hupumzika, na vali za semilunar hufunga kutokana na shinikizo la damu katika mshipa wa aota.

Katika mzunguko wa moyo, shinikizo la damu huongezeka na kupungua. Mzunguko wa moyo huratibiwa na mfululizo wa umeme unaozalishwa na chembechembe maalum za moyo zinazopatikana ndani ya nodi ya saino-atiria na node ya atirio-ventrikali. Misuli ya moyo inajumuishwa na chembechembe za misuli ambayo huanzisha mnyweo wao yenyewe bila msaada wa neva za nje (ukiondoa zile za kuboresha kiwango cha moyo kutokana na shughuli za mwili za kudumisha uhai). Katika hali ya kawaida, kila mzunguko huchukua wastani wa sekunde mbili.

Sistoli ya Atiria[hariri | hariri chanzo]

atirial sistoli

Sistoli ya Atiria ni mnyweo wa misuli ya moyo (myocardia) ya atiria ya kushoto na kulia. Kwa kawaida, atiria zote hunywea kwa wakati mmoja. Neno sistoli ni sawa na kunywea (kukama au kufupika) kwa misuli. Sistoli ya umeme ni shughuli ya umeme ambayo huchangamsha misuli ya vyumba vya moyo (myocardium) kunywea. Hii hufuatiwa punde na sistoli ya kimakanika, ambayo ni mnyweo halisi wa moyo.

Mnyweo wa atiria, husababisha shinikizo la damu kuongezeka katika kila atiria, na kulazimisha damu ya ziada kuingia kwenye ventrikali. Mtiririko huu wa damu ya ziada huitwa Kupiga kwa Atiria.

Asilimia 70 ya damu hutiririka kwenye ventrikali bila nguvu, hivyo atiria hazihitajiki kunywea kwa kiasi kikubwa. [3]

Kupiga kwa Atiria hukosekana kama kuna upungufu wa upitishaji wa umeme wa kawaida katika moyo, kama vile wakati wa mpapatiko wa atiria, mapigo ya atiria kwa kasi, na kuziba kwa moyo mzima. Hali ya kupiga kwa Atiria pia inatofautiana kulingana na hali ya moyo, kama vile moyo mgumu, hali ambayo hupatikana katika wagonjwa walio na kasoro katika utendakazi wa dayastoli (diastolic dysfunction).

Kugundua sistoli ya atiria[hariri | hariri chanzo]

Sistoli ya umeme ya atiria huanza na mwanzo wa wimbi P kwenye ECG. Wimbi la kuondoa kingamizi amabayo inafanya atiria zote mbili kunywea kwa wakati mmoja ni kutokana na nodi ya saino-atiria ambayo iko kwenye ukuta wa juu ya atiria ya kulia. Asilimia 30 ya ventrikali hujazwa katika awamu hii.

Sistoli ya Ventrikali[hariri | hariri chanzo]

Sistoli ya Ventrikali

Sistoli ya Ventrikali ni mnyweo wa misuli (myocardia) ya ventrikali ya kushoto na kulia.

Baadaye katika wakati wa kutoa damu kwa nguvu, ingawa shinikizo la ventrikali hushuka chini ya shinikizo la aota, bado vali ya aota hubaki wazi kwa sababu ya nguvu ya damu iliyotolewa. [4]

Grafu ya shinikizo la aota katika mzunguko wa moyo huonyesha mteremko kidogo ambao hulingana na kufunga kwa vali ya aota. Mteremko kwenye grafu hufuatiwa mara moja na kupanda kwa muda mfupi kisha kushuka taratibu. Kupanda kidogo kwa grafu hujulikana kama nochi ya "daikrotiki" au "mkato", na inawakilisha kuongezeza kwa muda mfupi katika shinikizo la aota. Ventrikali ikianza kuingia katika dayastoli, mtiririko mfupi wa damu kutoka aota kurudi kwenye ventrikali ya kushoto husababisha vali ya aota ya kufunga. Matokeo ni kuongezeka kidogo kwa shinikizo ya aota kwa sababu unyumbufu ya vali za semilunar na aota. [5] [6] [7]

Kugundua ya sistoli ya ventrikali[hariri | hariri chanzo]

Sauti za moyo[hariri | hariri chanzo]

Makala kuu: Heart sounds

Kufunga kwa vali za mitral na tricuspid (zinazojulikana kwa pamoja kama vali za atirioventrikali ) mwanzoni mwa sistoli ya ventrikali husababisha sehemu ya kwanza ya sauti ya "lubb-dubb" inayotolewa na mapigo ya moyo. Rasmi, sauti hiyo inajulikana kama Sauti ya kwanza ya Moyo, au S 1. Sauti hiyo ya kwanza hutolewa na kufunga kwa vali za mitral na tricuspid na ni sauti yenye sehemu mbili, M1 na T1.

Sehemu ya pili ya "lubb-dubb" (Sauti ya pili ya Moyo, au S 2), husababishwa na kufunga kwa vali za aorta na ateri ya mapafu mwishoni mwa sistoli ya ventrikali. Ventrikali ya kushoto ikiwa inatoa damu, shinikizo lake hushuka chini ya shinikizo katika aota, na vali ya aorta hufunga. Vile vile, shinikizo la ventrikali ya kulia ikishuka chini ya shinikizo la ateri ya mapafu, vali ya ateri ya mapafu hufunga. Satui ya pili ya Moyo, pia ina sehemu mbili, A2 na P2. Vali ya aota hufunga mapema kuliko vali ya ateri ya mapafu na hutenganishwa kwenye sauti ya pili ya moyo. Kutenganishwa huku kwa S2 husikika wakati wa kuvuta pumzi tu.

Mchoro wa uchunguzimeme wa moyo[hariri | hariri chanzo]

Katika mchoro wa uchunguzimeme wa moyo, sistoli ya umeme ya ventrikali huanza wakati wa mwanzo wa tata wa QRS.

Dayastoli[hariri | hariri chanzo]

Diastole ugonjwa wa moyo

Dayastoli ya Moyo ni wakati moyo hupumzika baada ya mnyweo kwa ajili ya maandalizi ya kujijaza na damu kutoka kwenye mzunguko. Dayastoli ya Ventrikali ni wakati ventrikali inapumzika, wakati dayastoli ya atiria ni wakati atiria inapumzika. Kwa pamoja hujulikana kama Dayastoli wa moyo mzima

Katika dayastoli ya ventrikali, shinikizo katika ventrikali (ya kushoto na kulia) hushuka kutoka kilele inachofika katika sistoli. Baada ya shinikizo katika ventrikali ya kushoto kushuka chini ya shinikizo atiria ya kushoto, vali ya mitral hufunguka, na ventrikali ya kushoto hujazwa na damu iliyokuwa inakusanyika katika atiria ya kushoto. Muda wa kupumzika yenye ujazo sawa ni muda kutoka sauti ya pili moyo, sehemu ya aota, yaani kufunga kwa vali ya aota, hadi mwanzo wa kujaza kwa sababu ya vali ya mitral kufungua. [8] Hali kadhalika, shinikizo kwenye ventrikali ya kulia ikishuka chini ya shinikizo kwenye atiria ya kulia, vali ya tricuspid hufunguka, na ventrikali ya kulia hujazwa na damu iliyojikusanyika kwenye atiria ya kulia. Wakati wa dayastoli, shinikizo ndani ya myocardium ni chini zaidi kuliko kwenye aota, ambayo inaruhusu damu kuzunguka ndani ya moyo yenyewe kupitia ateri ya koronari.

Urekebishaji wa mzunguko wa moyo[hariri | hariri chanzo]

Misuli ya moyo inauotomatiki, kumaanisha kwamba inaweza kujishtua. (Pia unaweza kuita kama "myogenic" tishu. Maana ni tishu yenye uwezo wa kujisisimua yenyewe.) Hii ni tofauti na misuli ya kiunzi cha mifupa, ambayo inahitaji aidha msisimko wa hiari au tendohiari kutoka kwa neva. Manyweo ya moyo kwa mdundo hutokea kwa hiari, ingawa kiwango cha manyweo zinaweza kubadilishwa na hamasa za neva au homoni, mazoezi na hisia. Kwa mfano, mfumo wa neva wa simpathetiki kwa moyo huongeza kiwango cha kasi ya moyo na neva ya vagus hupunguza kiwango cha moyo.

Manyweo ya moyo kwa mdundo hupatanishwa na nodi za sinoatriali (SA) na atriaventrikali (AV). Nodi ya sinoatirial, mara nyingi hujulikana kama kiongoza-mwendo wa moyo , hupatikana kwenye ukuta wa juu ya atiria ya kulia na husababisha mawimbi ya umeme ya kusisimua ambayo huanzisha mnyweo wa atiria kwa kutengeneza uwezo wa kutenda. Mara baada ya wimbi kufika nodi AV, ambayo iko kwenye atiria ya kulia upande wa chini, inacheleweshwa huko kabla ya kupitishwa kwenye Kifungu antriaventrikali na juu kwenye nyuzi za Purkinje, na hivyo husababisha mnyweo ya ventrikali. Ucheleweshaji kwenye nodi AV inaruhusu muda wa kutosha kwa ajili ya damu katika atiria kujaza ventrikali husika. Katika tukio la patholojia kali, nodi AV pia inaweza kufanya kazi kama kiongoza-mwendo, hii si kawaida kwa sababu ya kiwango cha kutoa mawimbi ni ndogo kuliko kile cha seli za kiongoza-mwendo kwenye nodi SA, kwa hiyo huzidiwa kiwango.

Tazama Pia[hariri | hariri chanzo]

  • Lango:Tiba
  • Kilele kuwapiga
  • Shinikizo la damu
  • Uwezo wa kutenda cha moyo
  • Misuli ya moyo
  • Uzalishaji wa moyo
  • Mchoro wa uchunguzimeme wa moyo
  • Moyo
  • Systolic array (usanifu wa kompyuta )
  • Ventrikali

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Mwendo wa moyo ni pendekezo la KyT
  2. Guyton, AC & Hall, Je (2006) Textbook of Medical Physiology (11 ed.) Philadelphia: Elsevier Saunder ISBN 0-7216-0240-1
  3. [1] ^ Advanced Biology for You - Gareth Williams
  4. [2] ^ Cardiovascular Physiology Concepts by Richard E. Klabunde, Ph.D.: Cardiac Cycle - Reduced Ejection (Phase 4)
  5. Plethysmograph
  6. Moyo. Jalada kutoka ya awali juu ya 2011-06-06. Iliwekwa mnamo 2010-09-06.
  7. [5] ^ Human Cardiopulmonary Physiology Archived 8 Juni 2011 at the Wayback Machine.
  8. [7] ^ Inductance cardiography (thoracocardiography): A novel, noninvasive technique for monitoring left ventricular filling. Journal of Care muhimu, Volume 14, Issue 4, Kurasa 177-185

Viunganishi vya nje[hariri | hariri chanzo]

'Nakala Jasiri'