Nenda kwa yaliyomo

Mwanaidi Mayowela

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwanaidi Mayowela
Nchi Tanzania
Kazi yake mjasiriamali

Mwanaidi Mayowela ni mwanamke mjasiriamali ambaye hapo awali alikuwa anaombaomba maeneo ya posta kulingana na changamoto ya viungo vya mwili wake (ulemavu)[1].

Kwa kuona ni kwa jinsi gani anaweza kujikwamua kimaisha kwa kutumia mikono yake, mwanamke huyu ndipo akajiunga na kikundi cha wamama wenzie waliokua wanajishuhulisha na kazi za mikono.

Mwanaidi Mayowela pia alionesha nia ya kutaka kufanya biashara yoyote ambayo ingeweza kumsaidia, aliweza kuanza kutengeneza bangili za asili (utamaduni) pamoja na mikoba ambayo alikuwa anauzia maeneo yale aliyokuwa anaombaomba[2].

Mnamo Aprili 2017 alipata Tuzo ya heshima na katika tuzo za Malkia wa Nguvu zinazoratibiwa na Clouds Media Group na washirika wake.[3]