Mimi ni Johnson Massawe. Humu hujiita "Jonny Frosty", ni kijana kutoka Dar es Salaam, Tanzania mwenye shauku kubwa ya teknolojia na ubunifu. Nina utaalamu katika mitandao ya kompyuta, usalama wa taarifa, usimamizi wa mifumo na hifadhidata, pamoja na ufundi wa vifaa na programu. Mbali na kazi za TEHAMA, ninashiriki kikamilifu kwenye miradi ya Wikimedia kama mratibu na mchangiaji, nikihamasisha na kuhifadhi maarifa huru kuhusu historia, utamaduni na urithi wa Tanzania na Afrika. “Teknolojia ni daraja la kesho, tuilinde na tuiendeleze.”