Mlinzi mzamaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mlinzi mzamaji
Mlinzi mzamaji mdogo (Pelecanoides urinatrix)
Mlinzi mzamaji mdogo (Pelecanoides urinatrix)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Procellariiformes (Ndege kama walinzi)
Familia: Procellariidae (Ndege walio na mnasaba na walinzi)
Jenasi: Pelecanoides
Lacépède, 1799
Spishi: P. garnotii (Lesson, 1828)

P. georgicus Murphy & Harper, 1916
P. magellani (Mathews, 1912)
P. urinatrix (Gmelin, 1789)

Walinzi wazamaji ni ndege wadogo wa bahari wa jenasi Pelecanoides, jenasi pekee ya familia Pelecanoididae. Wataalamu wengine huwaainisha katika familia Procellariidae (walinzi), lakini walinzi wazamaji ni wadogo kuliko walinzi wengine, wana mabawa mafupi na mirija ya pua inaelekea juu badala ya mbele. Wanatokea bahari za kusini na huzamia kabisa ili kuwakamata gegereka wadogo hasa (krili, kopepodi na amfipodi) na samaki na ngisi wadogo pia. Majike hulitaga yai moja tu ardhini katika makoloni kwenye visiwa vya mbali visipokaa watu wala mamalia wengine. Kwa kawaida huyatembelea makoloni yao usiku kuzuia shakwe-waporaji.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]