Majadiliano:Sungura pori

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Bwana Mwasapi, sifahamu kwa nini umechagua jina "sungura pori" kutafsiri jina la Kiingereza "hare" na "sungura" kutafsiri "rabbit". Yule wa pili unamwita hata "sungura wa kawaida" ijapokuwa "rabbits" hawatokei Afrika. "Hares" wanatokea Afrika, kwa hivyo kwa maoni yangu jina "sungura" lingekuwa chaguo la kwanza kwao. Kwa "rabbit" napenda zaidi "sungura-shimo". ChriKo (majadiliano) 22:57, 30 Machi 2010 (UTC)[jibu]

ChriKo, pole kwanza kwa kuingilia mjadala. BE, sidhani kama atakujibu tena kwa sababu huyu mwandishi ni yule wa ile orodha ya watu kitu, ukiwa huna kitu si mtu (wanafunzi walioshindania shindano la Wikipedia lililodhaminiwa na GOOGLE). Hivyo hatotokea tena. CHE, ni afadhali uchukue hatua inayofaa mwenyewe bila hata kushauriana naye - kwani hayupo tena. Pole mzee wangu. Wako,--MwanaharakatiLonga 07:02, 31 Machi 2010 (UTC)[jibu]
Muddyb, asante sana kwa kunieleza hii. Sasa nimefahamu. Salamu nyingi. ChriKo (majadiliano) 23:09, 31 Machi 2010 (UTC)[jibu]