Majadiliano:Fasihi simulizi

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Hadithi simulizi

Fasihi simulizi[hariri chanzo]

Fasihi simulizi ni aina ya fasihi inayotumia masimulizi ya mdomo katika uwasilishwaji wake.

  Dhima za fasihi simulizi

Kuelimisha jamii, Kuburudisha, Kutunza utamaduni na historia ya jamii, Kukuza lugha, Kukomboa jamii,

  Tanzu za fasihi simulizi

Fasihi simulizi ina tanzu kuu nne tanzu hizo ni 1.Hadithi 2.Semi 3.Ushaili 4.Sanaa za maonyesho

  1.Hadithi

Ni tungo zafasihi simulizi zitumiazolugha ya ujazo ya maongezi ya kila siku, masimulizi hayo hupangwa katika mtiririko wa vituko unaokamilisha kisa.Ili kisa kikamilike katika hadithi,hadithi huwa nawahusika kama vile binadamu na wanyamaambao ndio ni nyenzo ya kukiendesha kisa chenyewe .

  2.Semi

Ni fungu la tungo za fasihi simulizi ambazo ni fupifupi zenye kutumia picha,tamathali za semi na ishara.

  3.Ushaili

Ni fungu la fasihi simulizi linalojumuisha tungo zote zenye kutumia mapigo kwa utaratibu maalumu.

  4.Sanaa za maonyesho au sanaa za maigizo

Ni zinazoambatana na utendaji wa vitendo vya wahusika mbele ya hadhira.Mfano michezo ya majukwaani.

Asili ya fasihi simuulizi ni ipi?[hariri chanzo]

majibu tafadhari 41.93.80.33 08:50, 22 Machi 2023 (UTC)[jibu]