Kijichi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Kata ya Kijichi
Nchi Tanzania
Mkoa Dar es Salaam
Wilaya Temeke
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 69,195

Kijichi ni jina la kata ya Wilaya ya Temeke katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania yenye postikodi namba 15129[1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ina wakazi wapatao 69,195 waishio humo. [2]

Huko kuna shughuli za kilimo kama vile cha mchicha na hata kazi nyingine ndogondogo. Pia ni sehemu ambayo biashara nyingi hufanyika na maendeleo ya wakazi wa eneo hili si mabaya.

Kuna shule nyingi za serikali na za watu binafsi; za serikali za msingi ni shule za Kijichi, Bwawani, Mbagalaku; za watu binafsi za msingi ni Holy Cross Kamo, Praise Montfort na nyingine nyingi.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Temeke - Tanzania

Azimio | Buza | Chamazi | Chango'mbe | Charambe | Keko | Kibondemaji | Kiburugwa | Kijichi | Kilakala | Kilungule | Kurasini | Makangarawe | Mbagala | Mbagala Kuu | Mianzini | Miburani | Mtoni | Sandali | Tandika | Temeke | Toangoma | Yombo Vituka