Kasimwelekeo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kasimwelekeo (pia velositi[1] kutokana na Kiingereza velocity) ni kipimo cha kasi ya mwendo wa kitu kuelekea mahali fulani. [2]

Katika fizikia kasimwelekeo inataja muda unaohitajika kupeleka kitu kutoka mahali pamoja kwenda mahali pengine. Kwa hiyo ni kipimo kinachounganisha habari mbili yaani kasi na mwelekeo. Kipimo cha aina hii huitwa kipimo vekta.

Kwa mfano gari linaelekea kusini kwa kasi ya 70 km/h. Habari hizi kwa pamoja ni kasimwelekeo. [3]

+ mwelekeo.[2]

Kama kitu kinazunguka kwenye duara mara moja na kufikia pale kilipotoka hakikuondoshwa. Kwa hiyo uondoshaji wake ni = sifuri na hivyo hata kasimwelekeo ni sifuri. Hii ni tofauti na kasi ya kitu kile katika mwendo wa kuzunguka.

Kasimwelekeo ni lazima iwe na mwelekeo pia.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Kamusi ya TUKI KKK/ESD inataja "kasimwelekeo", TUKI-KAST inataja "velositi"
  2. 2.0 2.1 Physics Homework Help: Speed, Velocity, Acceleration. physics247.com. Iliwekwa mnamo 25 March 2010.
  3. Vectors, Introduction. id.mind.net. Iliwekwa mnamo 25 March 2010.[dead link]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kasimwelekeo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.