Kōyō Aoyagi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kōyō Aoyagi (青柳 晃洋, Aoyagi, Kōyō, amezaliwa 11 Desemba 1993) ni mchezaji wa besiboli mtaalamu kutoka Japani ambaye kwa sasa anacheza Hanshin Tigers ya Nippon kama mtaalamu wa besiboli.

Kōyō Aoyagi
Kōyō Aoyagi

Historia katika taaluma yake[hariri | hariri chanzo]

Kōyō alianza kucheza katika timu ya Terao Dolphins akiwa darasa la tano katika shule ya msingi, na kwenda kucheza katika timu ya Namamugi Junior High. Alikua mchezaji bora wa Shule ya Upili ya Kawasaki Kikoka huko Kanagawa, lakini timu yake haikuweza kufuzu kwa mashindano yoyote ya kitaifa.[1]

Aliingia Chuo Kikuu cha Teikyo ambapo alikuwa akianza katika timu yake katika Ligi ya Besiboli ya Chuo Kikuu cha Tokyo Metropolitan Area. Licha ya kufanyiwa upasuaji wa kiwiko cha mkono wa kulia katika mwaka wake wa tatu, alicheza vyema mwaka uliofuata ambapo aliongoza ligi, na kutunukiwa tuzo ya Tisa Bora.[2] Baada ya miaka minne alikuwa amecheza mara 37.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://en.wikipedia.org/wiki/Sports_Nippon
  2. "Daily Sports (Japanese newspaper)", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2021-09-13, iliwekwa mnamo 2021-12-03