James Brady

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Brady in 1986

James Scott Brady (Agosti 29, 1940 - 4 Agosti 2014) alikuwa afisa wa umma wa Marekani ambaye aliwahi kuwa msaidizi wa rais wa Marekani na katibu wa habari wa kumi na saba wa White House, akihudumu chini ya Rais Ronald Reagan. Mnamo 1981, Brady alipata ulemavu wa kudumu kutokana na jeraha la risasi wakati wa jaribio la kumuua Ronald Reagan, miezi miwili tu na siku 10 baada ya kuapishwa kwa Reagan.

Kazi yake ya mwanzo[hariri | hariri chanzo]

Brady alianza kazi yake mwanzo katika utumishi wa umma kama mfanyikazi katika ofisi ya seneta wa Illinois Everett Dirksen (R-IL). Mnamo 1964, alikuwa meneja wa kampeni ya mgombea wa ubunge Wayne Jones katika kinyang'anyiro cha Wilaya ya 23 ya Illinois. Mnamo 1970, Brady aliongoza kampeni katika wilaya hiyo hiyo kwa ajili ya Phyllis Schlafly.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]