Harakati za vijana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Harakati za vijana ni ushirikishwaji wa watu wenye umri kati ya miaka 15-24 katika kuandaa jamii kwa ajili ya mabadiliko[1].

Wanaharakati wachanga wamechukua nafasi za uongozi katika maandamano ya umma kuhusu masuala mengi kama mabadiliko ya hali ya hewa, utoaji mimba na vurugu za bunduki. [2]

Tofauti na maandamano pamoja na utetezi wa kipindi cha nyumba, teknolojia imekuwa uti wa mgongo kwenye harakati za vijana wa kisasa. [3] Imeonekana masomo mengi ambayo hutumia mtandao katika kutafuta taarifa imekuwa na matokeo chanya katika ushiriki wa kisiasa. [4] Mitandao maarufu ya kijamii kama Twitter, Instagram na Youtube imekuwa nyenzo mpya kwa wanaharakati wachanga kwenye karne ya 21. Teknolojia pamoja na matumizi ya mitandao ya kidijitali imebadilisha namna vijana wanavyoshiriki kwenye harakati duniani na vijana wamekuwa hodari zaidi kwenye mitandao tofauti na vizazi vya zamani.[5]

Muhtasari[hariri | hariri chanzo]

Ushiriki wa vijana kwenye siasa umekua kwa miaka 10 iliyopita. Hata hivyo vijana wengi ni wananchi husika na wenye taarifa ambao wanaweza kutetea mabadiliko ndani ya jamii zao. Vijana ni jamii nyumbufu ambayo huanza na kuishia kulingana na mitazamo ya kiutamaduni, lakini mara nyingi hatua ya pekee katika maisha ya mtu ambapo masuala mahususi au sera huwa muhimu sana. Hizi huweza kujumuisha masuala ya kisiasa, kiafya na kijamii.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]