Fugo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mbwa kaya anaaminiwa kuwa mnyama wa kwanza aliyetokwakwa njia ya fugo
Mbwa mwitu wa Ulaya alikuwa babu wa mbwa kaya

Fugo (ing. domestication kutoka lat. domesticus: "kuhusiana na nyumba") ni mchakato unaotoeka kama wanyama mwitu wanaishi karibu na watu na kufugwa nao kwa muda mrefu.

Uteuzi wa tabia za wanyama[hariri | hariri chanzo]

Katika muda wa vizazi vingi tabia mbalimbali za wanayama zinabadilika. Hii inatokea hasa kwa sababu watu waliteua wanyama wenye tabia zilizotakiwa, kwa mfano

  • ukali ya kupungukiwa
  • uvumulivu kwa kukaa karibu na binadamu
  • kiasi cha nyama au maziwa au sufu
  • uwezo wa kutumia chakula kilicholiwa na binadamu
  • idadi ya watoto na uwingi wa kuzaa

Katika mchakato wa uteuzi wanyama wasiolingana hawakupewa nafasi ya kuzaa tena yaani hawakufugwa na hivyo tabia zisizotakiwa zilipugua na tabia zilizotafutwa ziliongezeka.

Fugo kwa mimea[hariri | hariri chanzo]

Mchakato huohuo ulitokea pia upande wa mimea.

Watu walikuta manyasi yenye mbegu kubwa kiasi uliofaa kama chakula wakatambua ya kwamba waliweza kutunza mbegu za aina hii ya nyasi na kuzipanda mahali walipohamia wakaona wakitunza mbegu kubwa zaidi kwa kupanda polepole mimea mpya ikaota mbegu kubwa zaidi.

Katika mchakato huu kipo chanzo cha kutokea kwa nafaka zote zinazoliwa na binadamu. lakini pia mimea mingine ya matunda kama vile ndizi au mitofaa.


Kujisomea[hariri | hariri chanzo]


Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]