Doja Cat

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Amala Ratna Zandile Dlamini (Kuzaliwa Oktoba 21, 1995), hujulikana kitaalamu kama Doja Cat. ni rapper wa Kimarekani, mwimbaji, mtunzi wa nyimbo, na mtayarishaji wa rekodi. Alizaliwa na kukulia Los Angeles, Doja Cat alianza kutengeneza na kuachia muziki kupitia Sound Cloud. Wimbo wake "So High" ilivuta umakini wa Kemosabe na RCA Records ambayo alisaini mkataba wa pamoja wa rekodi. Alitoa EP yake ya kwanza Purrr! mwaka 2014.

Doja Cat akiwa Taiwan 2022

Baada ya kusitishwa kwa kutoa muziki na kutolewa kwa bahati mbaya kwa albamu yake ya kwanza ya studio, Amala (2018), Doja Cat alipata mafanikio ya kawaida kama meme yake ya mtandaoni kupitia nyimbo ya Mooo!, wimbo mpya ambapo yeye anatoa madai ya kejeli kuhusu kuwa ng'ombe. Kwa kutumia umaarufu wake unaokua, alitoa albamu yake ya pili ya studio, Hot Pink, mwaka uliofuata. Ilifikia 10 bora ya Billboard 200 ya Marekani na kutoa wimbo "Say So", na remix yake iliyomshilikisha Nick Minaj, ikiwa kinara kwenye Billiboard 100. Albamu yake ya tatu , iitwayo Planet Her(2021), alitumia wiki tatu mfululizo akiwa nambari mbili kwenye Billboard 200 na kuzaa nyimbo 10 bora zaidi "Kiss Me More" (akimshirikisha SZA), "Need to Know", na "Woman".

Imefafanuliwa na The Wall Street Journal kama "rapa stadi wa kiufundi na mwenye hisia kali za sauti na uwepo wa ujasiri wa kuona"[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "The Wall Street Journal", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2023-05-11, iliwekwa mnamo 2023-05-14