Cape Canaveral

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Coordinates: 28°28′N 80°32′E / 28.46°N 80.53°E / 28.46; 80.53

Kituo cha Kennedy Space Center huko Cape Canaveral

Cape Canaveral ni rasi ndogo kwenye pwani la Jimbo la Florida katika kusini mwa Marekani. Ni mashuhuri kama eneo ambako makombora na vyombo vya angani vya Marekani vilirushwa.

Katika eneo la Cape Canaveral kuna vituo viwili vinavyohusika na usafiri wa anga:

  • Kennedy Space Center (KSC) ya NASA na kutoka hapa vilirushwa vyombo vya angani vya Kimarekani vilivyobeba abiria, kama vile Saturn V na Space Shuttle.
  • Kituo cha Cape Canaveral cha jeshi la anga la US Air Force ambako makombora ya kubeba satelaiti na vipimaanga vimerushwa.

Kati ya 1963 hadi 1973 rasi ilibadilishwa jina ikaitwa "Cape Kennedy" lakini baadaye jina la awali likarudishwa.

Rasi hii iliteuliwa kwa ajili ya viwanja vya usafiri wa angani kwa sababu iko katika kusini ya Marekani hivyo karibu zadi na ikweta. Makombora yanahitaji nguvu na fueli kidogo kufika obiti kama yanarushwa karibu na ikweta ya Dunia.

Astrowiki.PNG
Mradi wa Astronomia Makala hii imewahi kukaguliwa na kuboreshwa kwenye warsha ya pamoja ya Jenga Wikipedia ya Kiswahili, Wikimedia Community User Group Tanzania na ASSAT. Imepewa hali ya ulinzi. Tunaomba mapendekezo yote ya usahihisho na nyongeza zipelekwe kwanza kwenye ukurasa wa majadiliano