Benki ya Dunia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Benki ya Dunia

Benki ya Dunia ni taasisi ya kimataifa yenye shabaha ya kusaidia maendeleo ya nchi za dunia. Si benki ya kawaida. Inashirikiana na Umoja wa Mataifa na hasa Shirika la Fedha la Kimataifa lakini si chini ya UM moja kwa moja. Ni mali ya nchi wanachama 185 zinazopigia kura katika mikutano yake kulingana na thamani ya hisa zao katika rasilmali ya benki.

Muundo wa Benki ya Dunia

Benki ya Dunia ina matawi mawili ambayo ni

Taasisi za ziada ambamo kila nchi mwanachama inapaswa kuingia pia ni

Makao makuu yapo Washington DC nchini Marekani. Kikatiba mwenyekiti wa benki ni mtu wa Marekani.

Hisa na kura

Maazimio hufuata kura za wanachama zinazolingana na idadi ya hisa za nchi hizo katika rasilmali ya benki (kwa mabano: IFC). Nchi zenye kura nyingi ni:

(Hali ya mwaka 2004)

Shabaha ya kazi

Benki (IBRD) inalenga kutoa mikopo kwa nchi zilizoendelea kiasi na pia nchi maskini zenye uwezo wa kulipia mikopo. Shirikisho la Maendeleo (IDA) inaangalia mahitaji ya nchi maskini kabisa.

Kwa jumla taasisi za Benki ya Dunia hutoa mikopo kwa riba ndogo au hata zisizo na riba halafu pia misaada zisizorudishwa kwa nchi maskini kwa kusudi la kujenga elimu, afya, barabara na mawasiliano.

Historia

Benki ilianzishwa mwaka 1945 baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Shabaha ilikuwa kusaidia nchi za Ulaya zilizoharibiwa katika vita. Mkopo wa kwanza wa milioni USD 250 ulitolewa kwa Ufaransa.


Viungo vya Nje