Nenda kwa yaliyomo

Beata Habyarimana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Beata Habyarimana
AmezaliwaBeata Uwamaliza Habyarimana
Kazi yakeMkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Bank of Kigali Group

Beata Uwamaliza Habyarimana (alizaliwa Septemba 1975) ni mtaalam wa uchumi na mshauri wa masuala ya kifedha kutoka nchini Rwanda. Wadhifa ambao anautumikia kwa zaidi ya miaka 16 ya uzoefu katika sekta ya fedha na taasisi za ndani ya Afrika na kimataifa. Eneo lake la umahiri linahusisha kubadilisha biashara na mabadiliko ya shirika.

Hivi sasa ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Bank of Kigali Group, taasisi kubwa ya kifedha nchini Rwanda yenye kampuni tanzu tano: huduma za Benki, Bima, Usimamizi wa Mali, Suluhisho za Kidijitali kupitia Techouse, na shughuli za Kifilantropia kupitia Asasi yao ya kiraia.[1]

Maisha ya awali na elimu

[hariri | hariri chanzo]

Beata alizaliwa mnamo Septemba 1975. Alipata shahada ya kwanza (Bachelor’s Degree) katika Fedha katika University of Rwanda kuanzia mwaka 1996 hadi 2000, na ana shahada ya uzamili katika Usimamizi wa Uchumi kutoka Maastricht University nchini Netherlands mwaka 2011.

  1. Akayezu Jean de Dieu (2021-07-18). "Umunyakuri wakabije inzozi, iby'igitabo cyamuhinduye: Byinshi ku buzima bwa Minisitiri Habyarimana (Video) - IGIHE.com". igihe.com (kwa Kinyarwanda). Iliwekwa mnamo 2024-12-29.