Vijana wa Kiafrika Amílcar Cabral

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

African Youth Amílcar Cabral (kwa KIreno:Juventude Africana Amílcar Cabral) ni tawi la vijana la PAIGC nchini Guinea Bisau. JAAC ilianzishwa mnamo Septemba 12, mwaka 1974, huko Boé.

Baada ya kutenganishwa kwa PAICV na PAIGC, sehemu ya Cape Verde ya JAAC ikawa shirika tofauti, pia inaitwa JAAC. Leo shirika hilo limepewa jina la Youth of PAICV (Juventude do PAICV).

JAAC ni mwanachama wa Shirikisho la Vijana wa Kidemokrasia Ulimwenguni, ingawa haifanyi kazi tena katika shirika hilo. Ilikuwa mwanachama wa Umoja wa Kimataifa wa Wanafunzi, lakini uanachama kwa sasa umegandishwa. JAAC imepata hadhi ya mwangalizi katika Umoja wa Kimataifa wa Vijana wa Kisoshalisti.